UVCCM E-TALK NA USHIRIKI WA VIJANA KATIKA UJENZI WA TAIFA
Dodoma | Januari 24, 2026 Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), kupitia jukwaa la mtandao UVCCM e-Talk, tarehe 24 Januari 2026, kuanzia saa 12:00 jioni hadi saa 2:00 usiku, uliendesha mjadala mpana wa kitaifa uliowakutanisha vijana kutoka maeneo mbalimbali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa lengo la kujadili nafasi na mchango wa vijana katika siasa na ujenzi wa taifa.
Soma Zaidi
VIJANA: TUPO TAYARI KUZIPOKEA FURSA ALIZOTUANDAA DKT. SAMIA” – VIJANA DODOMA
Dodoma. Maelfu ya wanafunzi kutoka vyuo vya kati na vyuo vikuu wamejitokeza kwa wingi leo tarehe 24 Januari, 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma, kushiriki Kongamano la UNI-Summit Life In & After Campus, linalolenga kuwajengea vijana uelewa wa kina kuhusu fursa mbalimbali zilizopo Serikalini na katika sekta binafsi.
Soma Zaidi
PPRA YAWAJENGEA UWEZO VIJANA KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA
Dodoma. Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) imeendelea kuchukua hatua za makusudi kuwajengea uwezo vijana ili washiriki kikamilifu katika mifumo ya ununuzi wa umma, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kukuza ushiriki wa vijana katika uchumi wa taifa.
Soma Zaidi
SERIKALI YATAJA MALENGO YA SERA YA MAENDELEO YA VIJANA (2007 – 2024)
Dodoma. Serikali kupitia Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana imeendelea kuweka msisitizo katika uwekezaji wa kimkakati kwa vijana, kwa kueleza maeneo muhimu ya Sera ya Maendeleo ya Vijana ya Mwaka 2007, Toleo la Mwaka 2024, yenye lengo la kumwezesha kijana kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.
Soma Zaidi
Kihongosi Apeleka Tabasamu Mashina ya CCM Singida
Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Kenani Laban Kihongosi, ameendelea na ziara yake ya kikazi mkoani Singida, ikiwa ni siku ya pili ya ziara hiyo, ambapo leo amepokelewa rasmi Wilaya ya Singida.
Soma Zaidi
Shina la Makunduchi Ladhihirisha kwa Vitendo Kuwa Maendeleo Hayana Itikadi – Dkt. Migiro
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Asha Rose Migiro, amezindua Shina la Wakereketwa wa CCM Makunduchi lililopo Mtaa wa Uhuru, Wilaya ya Dodoma Mjini, na kulipongeza shina hilo kwa kuwa mfano wa kuigwa katika kuendeleza shughuli za kiuchumi zinazolenga kuinua kipato cha wanajamii bila kujali misimamo ya kisiasa. Akizungumza na wajumbe wa shina hilo Januari 20, 2026, kabla ya kukutana na Mabalozi wa Mashina wa Mkoa wa Dodoma,
Soma Zaidi