UVCCM MJINI WAFANYA IFTAR GALA KWA MAFANIKIO MAKUBWA
Mjini, Unguja– Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Mjini umefanikiwa kuandaa hafla ya Iftar Gala iliyowakutanisha vijana kutoka maeneo mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya kuendeleza mshikamano, upendo na umoja miongoni mwa vijana wa chama hicho.
Soma Zaidi
DUA NA IFTARI YA PAMOJA ILIYOANDALIWA NA UVCCM KIGAMBONI YAFANA
Kigamboni, Dar es Salaam – Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Kigamboni umefanikiwa kuandaa hafla ya Dua na Iftari ya pamoja iliyowakutanisha vijana, viongozi wa chama na serikali, pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo katika mazingira ya mshikamano, ibada na mafunzo ya kijamii.
Soma Zaidi
RAIS DKT. MWINYI AFUTURISHA WANANCHI WA MKOA WA KUSINI PEMBA
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amejumuika na waumini wa dini ya Kiislamu na wananchi wa Mkoa wa Kusini Pemba katika futari ya pamoja aliyowaandalia. Hafla hiyo imefanyika leo tarehe 11 Machi 2026 katika Uwanja wa Kufurahishia Watoto Tibirinzi, Mkoa wa Kusini Pemba, ambapo pia imehudhuriwa na Mke wa Rais wa Zanzibar, Mama Mariam Mwinyi.
Soma Zaidi
DKT. SAMIA SHUJAA WA MAENDELEO NA USTAWI WA WANAWAKE TANZANIA
Na Mwandishi Wetu, Emmanuel Peter Frednand Tarehe 8 Machi ya kila mwaka dunia huadhimisha Siku ya Wanawake Duniani kwa lengo la kutambua mchango mkubwa na muhimu wa wanawake katika maendeleo ya jamii tunazoishi. Maadhimisho haya pia hutumika kutathmini hatua zilizopigwa katika kukuza usawa wa kijinsia na kuimarisha nafasi ya mwanamke katika nyanja mbalimbali za maendeleo.
Soma Zaidi
CCM na FRELIMO Kuimarisha Ushirikiano wa Kiuchumi
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Asha‑Rose Migiro, amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa FRELIMO wa Msumbiji, Chakil Felizardo Passadas Aboobacar, ambaye ameanza ziara rasmi ya kikazi ya siku mbili nchini Tanzania. Mazungumzo hayo yamefanyika leo tarehe 6 Machi 2026 katika Ofisi Ndogo za Makao Makuu ya CCM, Lumumba Offices,
Soma Zaidi
KATIBU MKUU UVCCM, HALID MWINYI AKAGUA MAENDELEO YA CHUO CHA VIJANA IHEMI – IRINGA
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Ndugu Halid Mwinyi, ametembelea na kukagua maendeleo ya Chuo cha UVCCM Ihemi kilichopo mkoani Iringa.
Soma Zaidi