KATIBU MKUU CCM DKT. ASHA ROSE MIGIRO: MABALOZI WA MASHINA NDIO SAUTI HALISI YA CHAMA
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha Rose Migiro, amewataka Mabalozi wa mashina kote nchini kuwa viongozi wenye uthubutu, dira na sauti, wasiobaki kuwa wapokeaji wa maelekezo kutoka juu pekee, bali wawe chimbuko la mawazo, maamuzi na maelekezo yanayopanda kutoka chini kwenda juu, kwani wao ndiyo wanaoishi na kuwatambua kwa karibu wanachama wa CCM.
Soma Zaidi
ZIARA YA KATIBU MKUU CCM DKT.ASHA -ROSE MIGIRO, KUKUTANA NA MABALOZI WA SHINA WA CCM
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Asha Rose Migiro, ameanza ziara yake ya kikazi katika Mkoa wa Dar es Salaam kwa kukutana na kuzungumza na mabalozi wa mashina ya CCM, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa uongozi wa Chama Cha Mapinduzi wa kuimarisha utendaji kuanzia ngazi ya chini.
Soma Zaidi
DKT. MIGIRO NI CHACHU YA MATUMAINI MAKUBWA KWA VIONGOZI WA MASHINA – MWENEZI KENANI
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa anayeshughulikia Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Ndugu Kenani Kihongosi, amesema Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Balozi Dkt. Asha Rose Migiro, ni chachu ya matumaini makubwa kwa viongozi wa mashina na wanachama wa chama hicho kutokana na uongozi wake wa mfano, unaojikita katika kulea, kufundisha na kuwaimarisha viongozi kuanzia ngazi ya chini
Soma Zaidi
Rais Samia Afanya Mazungumzo na Viongozi wa Wizara ya Ulinzi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya mazungumzo na Viongozi wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa katika Ikulu ndogo ya Tunguu, Zanzibar, tarehe 06 Januari, 2026. Mazungumzo hayo yalilenga kujadili masuala mbalimbali ya ulinzi, usalama wa taifa pamoja na mchango wa Jeshi la Kujenga Taifa katika maendeleo ya nchi.
Soma Zaidi
MATEMBEZI YA MAADHIMISHO YA MIAKA 62 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR YAANZA RASMI MKOA WA MJINI MAGHARIBI
Matembezi ya kuadhimisha Miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar yameanza rasmi leo katika Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja, yakihusisha makundi mbalimbali ya vijana, wanachama wa Chama Cha Mapinduzi pamoja na wananchi, waliokusanyika kuonesha mshikamano, uzalendo na heshima kwa historia ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Soma Zaidi
VIJANA VYUONI GOMBEENI UONGOZI UVCCM
Dodoma, 03 Januari 2026 – Katibu Msaidizi wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa, Vyuo na Vyuo Vikuu wa UVCCM, Ndugu Mabula Marco Mabula, amewahimiza vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaosoma katika vyuo na vyuo vikuu nchini kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya Seneti za Vyuo na Vyuo Vikuu kupitia jumuiya ya UVCCM.
Soma Zaidi