ZANZIBAR KUANZA USAFIRI WA MABASI YA UMEME MWISHONI MWA FEBRUARI 2026
Unguja – Zanzibar Zanzibar inatarajiwa kuanza rasmi usafiri wa umma wa kutumia mabasi ya umeme mwishoni mwa mwezi Februari, 2026, hatua itakayofungua ukurasa mpya katika sekta ya usafiri wa kisasa na rafiki kwa mazingira visiwani humo.
Soma Zaidi
BALOZI DK. ASHA-ROSE MIGIRO AFIKISHA SALAMU ZA RAIS DKT. SAMIA KWA WANANCHI WA KINONDONI NA UBUNGO
Ubungo / Kinondoni – Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, amewasilisha salamu za pongezi na shukrani kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa wananchi na wanachama wa CCM wa Wilaya za Ubungo na Kinondoni.
Soma Zaidi
MWENYEKITI KAWAIDA AONGOZA MATEMBEZI YA KUADHIMISHA MIAKA 62 YA MAPINDUZI MATUKUFU YA ZANZIBAR, KUSINI PEMBA
Na Mwandishi wetu, Kusini Pemba. Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Ndugu Mohammed Ali Kawaida (MCC), leo Ijumaa tarehe 09 Januari, 2026 ameongoza maelfu ya vijana katika Matembezi ya Amani ya kuadhimisha Miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yaliyofanyika katika Mkoa wa Kusini Pemba.
Soma Zaidi
KAWAIDA AWASILI PEMBA KUFUNGA MATEMBEZI YA MAADHIMISHO YA MIAKA 62 YA MAPINDUZI MATUKUFU YA ZANZIBAR
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Mohammed Ali Kawaida, amewasili katika Kisiwa cha Pemba kwa ajili ya kuongoza na kufunga matembezi ya maelfu ya vijana kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Miaka 62 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Soma Zaidi
KATIBU MKUU CCM DKT. ASHA ROSE MIGIRO: MABALOZI WA MASHINA NDIO SAUTI HALISI YA CHAMA
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Asha Rose Migiro, amewataka Mabalozi wa mashina kote nchini kuwa viongozi wenye uthubutu, dira na sauti, wasiobaki kuwa wapokeaji wa maelekezo kutoka juu pekee, bali wawe chimbuko la mawazo, maamuzi na maelekezo yanayopanda kutoka chini kwenda juu, kwani wao ndiyo wanaoishi na kuwatambua kwa karibu wanachama wa CCM.
Soma Zaidi
DKT. MIGIRO NI CHACHU YA MATUMAINI MAKUBWA KWA VIONGOZI WA MASHINA – MWENEZI KENANI
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa anayeshughulikia Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Ndugu Kenani Kihongosi, amesema Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Balozi Dkt. Asha Rose Migiro, ni chachu ya matumaini makubwa kwa viongozi wa mashina na wanachama wa chama hicho kutokana na uongozi wake wa mfano, unaojikita katika kulea, kufundisha na kuwaimarisha viongozi kuanzia ngazi ya chini
Soma Zaidi