UVCCM
Tafadhali subiri...
UMOJA WA VIJANA WA CCM (UVCCM)

UVCCM SUMBAWANGA YAADHIMISHA MIAKA 49 YA CCM KWA SHUGHULI ZA KIJAMII

31 Jan, 2026 60 Machapisho
SUMBAWANGA MJINI
Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Sumbawanga Mjini wameadhimisha miaka 49 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kushiriki katika shughuli mbalimbali za kijamii, ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono misingi ya chama ya kujitolea kwa jamii, amani na mshikamano wa kitaifa.
Maadhimisho hayo yalifanyika Januari 31, 2026, yakiongozwa na Katibu wa Vijana wa CCM Wilaya ya Sumbawanga Mjini, Ndugu Beatrice Ngonyani, ambapo vijana hao walifanya usafi katika Kituo cha Afya Mazwi, kuchangia damu kwa ajili ya kuokoa maisha ya wananchi, pamoja na kushiriki mchezo wa kirafiki wa mpira wa miguu dhidi ya watumishi wa Manispaa ya Sumbawanga.
Kupitia shughuli hizo, UVCCM Sumbawanga Mjini ilionesha kwa vitendo dhamira ya vijana wa CCM katika kushiriki ujenzi wa jamii na kudumisha mahusiano mema kati ya vijana, wananchi na taasisi za umma.
 “TUMECHAGUA UMOJA NA AMANI KWA MAENDELEO YA TAIFA LETU.”