UVCCM
Tafadhali subiri...
UMOJA WA VIJANA WA CCM (UVCCM)

UVCCM MUHEZA YAADHIMISHA MIAKA 49 YA CCM KWA VITENDO

31 Jan, 2026 81 Machapisho
MUHEZA, TANGA
UVCCM Wilaya ya Muheza, chini ya uongozi wa Mwenyekiti wake, Ndugu Aziza Mshakangoto, imeadhimisha miaka 49 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa vitendo vya kijamii na kuonesha mshikamano wa kijamii.
Maadhimisho hayo yamejumuisha kutembelea miradi ya maendeleo, kushiriki shughuli za kijamii, pamoja na kuonyesha utu na upendo kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika Shule ya Sekondari Mlingano.
Kwa miaka 49, CCM inaendelea kuthibitisha kuwa kazi inaonekana na utu unaishi, huku UVCCM ikisisitiza umuhimu wa vijana kushiriki katika kuendeleza jamii na kudumisha mshikamano wa kitaifa.
#KaziNaUtu #TunasongaMbele