SERIKALI KUKAMILISHA TAWI LA CHUO KIKUU CHA UDSM KAGERA
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya CCM, Ndugu Samia Suluhu Hassan akiwa Bukoba Mjini, Mkoa wa Kagera, amesema kuwa Serikali itaendelea kuwekeza katika elimu ya juu kwa kukamilisha tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Kagera hatua itakayokuza fursa za elimu, kuongeza utafiti na kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Ukanda wa ziwa.
Soma Zaidi
SERIKALI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA BARABARA KAGERA
Akiwa Bukoba Mjini Mkoa wa Kagera, Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameonesha dhamira thabiti ya kuendeleza uboreshaji wa miundombinu ya barabara ili kufungua fursa zaidi za kiuchumi, kurahisisha usafirishaji wa mazao na huduma, pamoja na kuunganisha vijiji na miji kupitia barabara za kisasa.
Soma Zaidi
MKUU WA MKOA WA SONGWE AFURAHISHWA NA UBUNIFU WA UVCCM KUPITIA MFUMO WA “KIJANI ILANI CHATBOT
Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mheshimiwa Jabiri Omari Makame, ametembelea banda la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) katika Maonesho ya Wiki ya Vijana Kitaifa yaliyotamatika katika Viwanja vya Uhindini Jijini Mbeya leo tarehe 14 Oktoba 2025 na kutoa pongezi kwa ubunifu wa kidijitali uliofanywa na vUVCCM chini ya uongozi bora wa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Ndugu Mohamed Ali Kawaida (MCC).
Soma Zaidi
JESSICA MSHAMA AONGOZA MATEMBEZI YA HAMASA MULEBA
Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi wa UVCCM Taifa, Ndg. Jessica Mshama, ameongoza matembezi ya maelfu ya vijana wa hamasa wilayani Muleba, mkoani Kagera, leo tarehe 15 Oktoba 2025, kuelekea kwenye mkutano wa hadhara wa Mgombea wa Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Soma Zaidi
MRADI WA MAJI WA ZIWA VIKTORIA KUWANUFAISHA WANAMULEBA
Ahadi za Dkt. Samia Suluhu Hassan zinaendelea kutafsiriwa kwa vitendo kupitia utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati inayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja, ikiwemo mradi wa maji safi na salama kutoka Ziwa Viktoria unaoelekezwa hadi Wilaya ya Muleba.
Soma Zaidi
SERIKALI KUKAMILISHA UJENZI WA CHUO CHA VETA KYAKA
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika Mkutano wa kampeni Uliofanyika Muleba, ameeleza dhamira ya Serikali kukamilisha ujenzi wa Chuo cha VETA Kyaka, hatua itakayowezesha vijana wa Kagera kupata mafunzo bora ya ufundi stadi na kujiajiri.
Soma Zaidi