VIJANA SHINYANGA WAFUNIKA, WAMUAPISHA DKT. SAMIA KWA KISHINDO CHA OKTOBA TUNATIKI
11 Oct, 2025
15 Machapisho
🗓️ Tarehe 11/10/2025
📍kahama-Shinyanga
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Mohammed Ali Kawaida (MCC), ameongoza maelfu ya vijana wa Shinyanga Mjini katika matembezi ya kishindo yaliyojaa hamasa, uzalendo na mshikamano chini ya kaulimbiu ya Oktoba Tunatiki Vijana hao wameonesha umoja wa nguvu ya kizazi kipya, wakiahidi kulinda amani, kudumisha utulivu wa Taifa na kujitoa kwa dhati kumpigia kura Dkt. Samia Suluhu Hassan tarehe 29 Oktoba 2025, wakisema ndiye kiongozi anayewaletea matumaini, Maendeleo,na Tanzania yenye usawa kwa wote.
Katika tukio hilo lililogeuka kuwa sherehe ya umoja na matumaini ya vijana, sauti za “Tunatiki!” zilitawala mitaa yote ya Shinyanga, zikibeba ujumbe wa imani kwa uongozi wa Dkt. Samia na ahadi ya kuendeleza juhudi zake za kujenga Tanzania yenye fursa, ajira na ustawi wa vijana Shinyanga imetoa Taswira ya Taifa lililo tayari kwa uchaguzi wa amani, huku vijana wakiahidi kuendelea kuwa nguzo imara ya ushindi wa CCM na uendelevu wa maendeleo chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan.
#OktobaTunatiki✅✅✅
#FyuchaBilaStresi
#TokaNiTokeTukaTiki✅
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.