UVCCM WILAYA YA KAKONKO WAFANYA MAADHIMISHO YA MIAKA 49 YA KUZALIWA KWA CCM
- Usafi na huduma kwa wagonjwa: Vijana wa UVCCM walishiriki katika usafi wa maeneo ya Zahanati ya Kasuga na kutembelea wagonjwa walioko Zahanati hiyo.
- Kuheshimu wazee: Kutembelea wazee na kutoa zawadi mbalimbali katika vitongoji vya Kewe, Mjini A, Kaganyi, na Kiomoka, wakionyesha heshima na upendo kwa wazee.
- Kupanda miti: Shule ya Msingi na Zahanati ya Kasuga zilipandwa miti kwa lengo la kudumisha mazingira na kukuza elimu ya utunzaji wa mazingira.
Habari Zinazohusiana
UVCCM MBEYA MJINI YAADHIMISHA MIAKA 49 YA CCM KWA SHUGHULI ZA KIMAENDELE MBEYA MJINI
31 Jan, 2026
Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Mbeya Mjini ameshiriki leo katika shughuli za kimaendeleo katika Kata ya Nzovwe, pamoja na Diwani wa kata hiyo. Shughuli zilizofanyika ni pamoja na kukarabati barabara na kujaza vifusi katika maeneo korofi, hatua zilizolenga kuboresha miundombinu ya wananchi na kuendeleza huduma za kijamii.
UVCCM Ngome waadhimisha Kuzaliwa CCM kwa Vitendo, wasafisha Soko la Ngome Iringa
31 Jan, 2026
Vijana wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Tawi la Ngome, Kata ya Kihesa, Wilaya ya Iringa Mjini mkoani Iringa, wamefanya shughuli ya usafi wa mazingira katika Soko la Ngome kama sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya siku ya kuzaliwa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).
ABUYA AWEKA MSISITIZO KWA VIJANA WA CCM KUKITETEA CHAMA NA VIONGOZI WAKE
31 Jan, 2026
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Kigoma, Ndugu Emanuel Abuya, amewataka vijana wa CCM kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kutetea, kulinda na kudumisha misingi, sera na uongozi wa Chama Cha Mapinduzi, akisisitiza kuwa hilo ni jukumu la msingi na la kihistoria kwa jumuiya ya vijana.