DKT SAMIA AKIONGEA NA WAPIGA KURA WAKE SHINYANGA MJINI
11 Oct, 2025
12 Machapisho
🗓️ Tarehe 11/10/2025
📍 Shinyanga -Tanzania
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daktari Samia Suluhu Hassan, ameendelea na kampeni zake kwa kishindo akiwa Shinyanga Mjini, ambako amezungumza na Maelfu ya wananchi waliokusanyika kumsikiliza, Akiwa jukwaani Dkt. Samia amesisitiza dhamira ya serikali ya awamu ya sita kuendeleza utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo barabara, maji, afya, elimu na nishati ambayo Imeleta Mapinduzi makubwa katika maisha ya wananchi wa Shinyanga.
Amehimiza pia umuhimu wa amani, umoja na mshikamano wa kitaifa kama nguzo kuu ya Maendeleo na Ustawi wa Taifa, Daktari Samia amewataka wananchi waendelee kuiamini CCM kwa vitendo vyake, Wakitambua kuwa Chama hicho kimekuwa chachu ya Maendeleo halisi yanayoonekana kote nchini, huku akiwahimiza wapiga kura wote kutoka, kutikisa na kutiki CCM Tarehe 29 Oktoba 2025 ili Kuendeleza Safari ya Maendeleo Isiyoacha mtu Nyuma.
#OktobaTunatiki ✅ ✅ ✅
#Fyuchabilastress
#TokaNitokeTukatiki ✅
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.