DKT.NCHIMBI AENDELEA KUSAKA KURA ZA USHINDI WA KISHINDO ZA DKT.SAMIA JIJINI DAR
30 Sep, 2025
26 Machapisho
Mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwahutubia Wananchi kwenye mkutano wake wa hadhara wa kampeni,uliofanyika leo Septemba 30,2025 katika uwanja wa Kampala-Gongolamboto,Jimbo la Ukonga wilaya ya ilala,jijini Dar es Salaam.
Akiwa katika viunga vya Kampala-Ukonga,Dkt.Nchimbi amewahutubia Wananchi huku akinadi Sera na Ilani ya chama hicho ya 2025-2030 yenye kulenga kuimarisha na kupeleka maendeleo kwa Wananchi.
Aidha, baada ya kuhutubia Wananchi,Dkt.Nchimbi pia alipata nafasi ya kuwanadi baadhi ya wagombea Ubunge wa mkoa huo akiwemo mgombea
Ubunge wa jimbo la Ukonga,Ndugu Jerry William Silaa, mgombea Ubunge wa jimbo la Kivule Ndugu Dougras Didas Masaburi na Madiwani.
Dkt.Nchimbi ni Mgombea mwenza wa Dkt Samia Suluhu Hassan katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025 wakipeperusha bendera ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambapo mkoa wa Dar es Salaam unakuwa wa 15 kufikiwa na Dkt Nchimbi katika kusaka kura za ushindi wa Kishindo za Mgombea Urais wa chama hicho Dkt.Samia Suluhu Hassan,Wabunge pamoja na Madiwani.
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.