📝VIJANA WAZANZIBAR WAFUNGULIWA MILANGO YA AJIRA ZA KIMATAIFA
19 Sep, 2025
16 Machapisho
⏰Ijumaa Tar,19/09/2025
🔛 Zanzibar-Tanzania
Ilani ya CCM 2025–2030 inaleta matumaini mapya kwa vijana wa Zanzibar kupitia mpango Kabambe wa Ajira Kupitia ushirikiano wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Wizara ya Mambo ya Nje, mikakati madhubuti imewekwa kuhakikisha vijana wanapata nafasi za ajira ndani na nje ya nchi.
CCM imejipanga kwa vitendo kwa kuendeleza mikataba ya ajira baina ya Tanzania na Mataifa mbalimbali duniani Hatua hii inalenga kuongeza fursa za ajira zenye Staha, kuimarisha ujuzi wa vijana na kupanua upeo wa kipato kwa familia nyingi za Kitanzania, hasa vijana Wanaohitimu elimu ya juu na mafunzo ya ufundi.
Kwa dira hii, vijana wa Zanzibar hawatabaki nyuma tena Ajira za kimataifa zitakuwa chachu ya maendeleo, zikijenga kizazi chenye matumaini, heshima na uwezo wa kushindana katika Soko la dunia, Ni wakati wa kuamini, kushirikiana na kutekeleza kwa vitendo falsafa ya Oktoba Tunatiki, Kijani Tumetulia, Fyucha Bila Stresi.
#KaziNaUtuTunasongaMbele
#OktobaTunatiki
#FyuchaBilaStresi
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.