JE, UMEUONA MKONO WA MAMA ITIGI-SINGIDA?
09 Sep, 2025
42 Machapisho
Leo ni siku ya kihistoria kwa wananchi wa Itigi, Singida, ambao wamejumuika kwa Shauku kubwa kumpokea Dkt Samia Suluhu Hassan Mgombea wa Urais aliyeonyesha nyuso za furaha, akiwapungia mikono wananchi na wakazi wa Itigi, akionyesha ukaribu na upendo kwa kila mmoja, Sasa ni wakati wa kuungana, kuimarisha mshikamano wa wananchi na kuonyesha upendo kwa Maendeleo.
Katika mkutano huu wa kampeni, wananchi walipata nafasi ya kusikia kwa ukaribu sera na mipango ya maendeleo inayolenga kuboresha maisha ya kila Mwana-Itigi,Singida na Taifa Kwa Ujumla, Ukitiki Kwa Mama Umetiki Kwa Maendeleo Bila Stresi,.
Ni hakika kuwa uongozi wa Mama Dkt Samia Suluhu Hassan Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania Kwa Tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM unalenga kuhakikisha kila sekta ya kijamii na kiuchumi inasonga mbele Kutoa elimu bora, afya kwa wote, kilimo cha kisasa, miundombinu ya barabara na maji hadi uwezeshaji wa vijana na wanawake yote yameelezwa kwa uwazi na shauku, Wananchi wa Itigi wamepata motisha na matumaini mapya ya maisha bora kupitia mpango huu wa maendeleo.
#KaziNaUtuTunasongaMbele
#OktobaTunatiki
#FyuchaBilaStresi
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.