ZANZIBAR YANG'ARA : CCM GALA DINNER 2025 ZACHANGWA BILIONI 5.93
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameongoza kwa kishindo hafla ya “CCM Gala Dinner 2025†iliyofanyika katika ukumbi wa Golden Tulip – Zanzibar, mnamo Agosti 17, 2025 kuanzia saa 11 jioni.
Baada ya mafanikio makubwa ya Gala Dinner ya Bara, sasa mwenge wa mshikamano na mshereheko umeendelea Visiwani Zanzibar kwa kishindo kikubwa. Hafla hii maalumu ya harambee imewaleta pamoja viongozi, vijana, wanachama na wadau mbalimbali walioujaza ukumbi kwa mapenzi ya dhati kwa chama chao kipenzi.
Katika tukio hilo la kihistoria, CCM imefanikiwa kuchangisha jumla ya Shilingi Bilioni 5.93, ikidhihirisha imani kubwa na mshikamano wa watanzania kuelekea ushindi wa chama katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Mapenzi makubwa kwa viongozi wetu
Wanachama na wananchi walionekana kwa hamsa kubwa, wakimpa heshima na mapenzi ya dhati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi wakionyesha mshikamano na imani kubwa kwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kukipongeza Chama Cha Mapinduzi kwa uongozi wake bora. Vijana walijitokeza kwa wingi, wakichangia kwa hamasa kubwa na kuonyesha kuwa ndilo jeshi kubwa la ushindi wa CCM.
Hamasa ya kuchangia inaendelea
Mchango wa Zanzibar umekuwa ni ishara ya nguvu ya chama. Wananchi wanaendelea kuchangia kwa kasi kubwa kila kona ya nchi kuhakikisha chama kinajipanga ipasavyo kuelekea uchaguzi mwezi oktoba 2025.
👉 Jinsi ya Kuchangia kupitia Simu
-
Piga:
*150*50*1# -
Ingiza Control Number:
C02025 -
Weka Kiasi cha Mchango
-
Ingiza PIN yako kuthibitisha
📌 Michango itaendelea kupokelewa hadi Agosti 27, 2025 – kila mchango wako ni nguvu ya ushindi wa CCM na dhamira ya maendeleo kwa kila Mtanzania,Tuendelee kuchangia kwa kasi
Habari Zinazohusiana
UVCCM WILAYA YA KAKONKO WAFANYA MAADHIMISHO YA MIAKA 49 YA KUZALIWA KWA CCM
01 Feb, 2026
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Kakonko umefanya maadhimisho ya kipekee kuelekea miaka 49 ya kuzaliwa kwa CCM, yatakayofanyika rasmi tarehe 5 Februari 2026. Maadhimisho haya yamejumuisha shughuli mbalimbali za kijamii zenye lengo la kuunga mkono maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla.
UVCCM Mufindi yaadhimisha Miaka 49 ya CCM kwa Baraza maalum, yasifu Mchango wa Vijana katika kutafuta ushindi kwa CCM
31 Jan, 2026
Katika kuelekea maadhimisho ya miaka 49 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Wilaya ya Mufindi umeanza maadhimisho hayo kwa kufanya baraza maalum lenye lengo la kuwapongeza na kuwashukuru vijana wa chama kwa mchango wao mkubwa katika kazi ya kutafuta kura wakati wa Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba mwaka jana.
ABUYA AWEKA MSISITIZO KWA VIJANA WA CCM KUKITETEA CHAMA NA VIONGOZI WAKE
31 Jan, 2026
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Kigoma, Ndugu Emanuel Abuya, amewataka vijana wa CCM kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kutetea, kulinda na kudumisha misingi, sera na uongozi wa Chama Cha Mapinduzi, akisisitiza kuwa hilo ni jukumu la msingi na la kihistoria kwa jumuiya ya vijana.