MAELFU WAJITOKEZA KUMSINDIKIZA DKT.SAMIA KUCHUKUA FOMU
Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na mgombea mwenza wake Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, wamechukua rasmi fomu za kugombea nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Tukio hilo limefanyika , Agosti 9, 2025, katika Ofisi za Tume Huru ya Uchaguzi (INEC) zilizopo Njedengwa, Dodoma.
Mapokezi ya Kishindo
Maelfu ya wananchi, wanachama na wapenzi wa CCM kutoka kila pembe ya Tanzania Bara na Visiwani walijitokeza kwa wingi kwa mapenzi na imani yao kubwa kwa mgombea wao Dkt. Samia. Viwanja vya Makao Makuu ya CCM – Dodoma vilifurika umati wa watu waliobeba mabango zenye jumbe za kuhamasisha ushindi wa chama, huku wakipaza sauti za kumshangilia Rais Samia na mgombea mwenza wake. Wananchi walikuwa wenye furaha kubwa baada ya kuona Dkt.Samia kachukua fomu
Barabara kuu za Dodoma zilijaa wananchi waliokuwa wakisubiri kwa hamu msafara wa wagombea wetu, wengi wakiwa na mabango yenye ujumbe wa kishindo kama vile:“Oktoba Tunakiti!â€â€œSamia ni Tumaini la Watanzaniaâ€â€œDkt Samia Chaguo letu†“Kazi na utu,tunasonga mbele", n.k
Ushuhuda wa mapenzi na imani ya wananchi
Wakati wa tukio hilo, ilidhihirika wazi kuwa watanzania wana imani kubwa na mapenzi ya dhati kwa CCM na mgombea wake Dkt. Samia, ambaye ameendelea kuaminika kutokana na uongozi wake bora wa kidiplomasia na wa maendeleo endelevu.
Kwa upande wake, Mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliwashukuru wananchi wote kwa kujitokeza kwa wingi na kusimama bega kwa bega na chama chao. Aliahidi kuendeleza kasi ya maendeleo, mshikamano wa kitaifa na ujenzi wa Taifa lenye matumaini makubwa kwa sasa na baadaye
Habari Zinazohusiana
UVCCM WILAYA YA KAKONKO WAFANYA MAADHIMISHO YA MIAKA 49 YA KUZALIWA KWA CCM
01 Feb, 2026
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Kakonko umefanya maadhimisho ya kipekee kuelekea miaka 49 ya kuzaliwa kwa CCM, yatakayofanyika rasmi tarehe 5 Februari 2026. Maadhimisho haya yamejumuisha shughuli mbalimbali za kijamii zenye lengo la kuunga mkono maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla.
ABUYA AWEKA MSISITIZO KWA VIJANA WA CCM KUKITETEA CHAMA NA VIONGOZI WAKE
31 Jan, 2026
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Kigoma, Ndugu Emanuel Abuya, amewataka vijana wa CCM kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kutetea, kulinda na kudumisha misingi, sera na uongozi wa Chama Cha Mapinduzi, akisisitiza kuwa hilo ni jukumu la msingi na la kihistoria kwa jumuiya ya vijana.
UVCCM Mufindi yaadhimisha Miaka 49 ya CCM kwa Baraza maalum, yasifu Mchango wa Vijana katika kutafuta ushindi kwa CCM
31 Jan, 2026
Katika kuelekea maadhimisho ya miaka 49 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Wilaya ya Mufindi umeanza maadhimisho hayo kwa kufanya baraza maalum lenye lengo la kuwapongeza na kuwashukuru vijana wa chama kwa mchango wao mkubwa katika kazi ya kutafuta kura wakati wa Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba mwaka jana.