CCM YAANZA HARAMBEE YA UCHAGUZI: WANANCHI WAIPOKEA KWA MIKONO MIWILI
Chama Cha Mapinduzi (CCM) tumezindua rasmi harambee ya kuchangia kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 na kufanikisha kukusanya Shilingi Bilioni 86.31 katika uzinduzi uliofanyika Agosti 12, 2025, katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam.
Uzinduzi huu umepokelewa kwa shangwe na wananchi, wafanyabiashara, wadau wa maendeleo na wanachama wa CCM, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Chama, Rais Samia Suluhu Hassan. Katika harambee hiyo, Rais Samia alichangia Sh. Milioni 100, huku Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, akichangia Sh. Milioni 50.
Jumla ya fedha taslimu zilizokusanywa ni Sh. Bilioni 56.31, huku Sh. Bilioni 30.2 zikiwa ahadi. Hii ni sehemu ya lengo kubwa la chama kukusanya Sh. Bilioni 100 kwa ajili ya maandalizi ya ushindi wa kishindo wa CCM katika uchaguzi wa 2025.
Akizungumza baada ya kupokelewa kwa michango hiyo, Rais Samia alisema:
“Kutoa ni moyo siyo utajiri. Michango yenu ndiyo ngao ya ushindi wetu na dhamira ya kuwaletea Watanzania maendeleo ya kweli.â€
Aidha, aliwahimiza wananchi wote kuendelea kushiriki harambee hii, wakiwemo Watanzania waishio nje ya nchi (Diaspora).
👉 Jinsi ya Kuchangia kupitia Simu:
-
Piga:
*150*50*1# -
Ingiza Control Number:
C02025 -
Weka Kiasi cha Mchango
-
Ingiza PIN yako kuthibitisha
Michango hii itaendelea kupokelewa hadi Agosti 27, 2025. Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dk. Emmanuel Nchimbi, amewahimiza Watanzania wote wenye mapenzi mema kuendelea kushiriki, akisisitiza kuwa hatua hii ni muhimu katika kuandaa ushindi wa chama kinachobeba matumaini ya wananchi
Habari Zinazohusiana
UVCCM WILAYA YA KAKONKO WAFANYA MAADHIMISHO YA MIAKA 49 YA KUZALIWA KWA CCM
01 Feb, 2026
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Kakonko umefanya maadhimisho ya kipekee kuelekea miaka 49 ya kuzaliwa kwa CCM, yatakayofanyika rasmi tarehe 5 Februari 2026. Maadhimisho haya yamejumuisha shughuli mbalimbali za kijamii zenye lengo la kuunga mkono maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla.
ABUYA AWEKA MSISITIZO KWA VIJANA WA CCM KUKITETEA CHAMA NA VIONGOZI WAKE
31 Jan, 2026
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Kigoma, Ndugu Emanuel Abuya, amewataka vijana wa CCM kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kutetea, kulinda na kudumisha misingi, sera na uongozi wa Chama Cha Mapinduzi, akisisitiza kuwa hilo ni jukumu la msingi na la kihistoria kwa jumuiya ya vijana.
UVCCM Mufindi yaadhimisha Miaka 49 ya CCM kwa Baraza maalum, yasifu Mchango wa Vijana katika kutafuta ushindi kwa CCM
31 Jan, 2026
Katika kuelekea maadhimisho ya miaka 49 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Wilaya ya Mufindi umeanza maadhimisho hayo kwa kufanya baraza maalum lenye lengo la kuwapongeza na kuwashukuru vijana wa chama kwa mchango wao mkubwa katika kazi ya kutafuta kura wakati wa Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba mwaka jana.