RAIS SAMIA ATWAA TUZO YA KIMATAIFA YA MAJI
Johannesburg, Afrika Kusini – 14 Agosti 2025:
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametunukiwa Tuzo ya Kimataifa ya Maji – Presidential Water Changemakers Award 2025 na Global Water Partnership kwa kushirikiana na Umoja wa Afrika. Hafla ya tuzo hiyo imefanyika katika Mkutano wa Uwekezaji katika Sekta ya Maji Afrika (AU–AIP Africa Water Investment Summit 2025) unaoendelea jijini Johannesburg kuanzia tarehe 13–15 Agosti 2025.
Tuzo hii imetolewa kwa kutambua mchango wa kipekee wa Rais Dkt. Samia katika kuongoza mageuzi makubwa ya sekta ya maji nchini Tanzania, hatua ambazo zimeboresha upatikanaji wa huduma hiyo muhimu kwa wananchi wa mijini na vijijini.
Chini ya uongozi wake:
- Upatikanaji wa maji vijijini umeongezeka kufikia 79.6%
- Upatikanaji wa maji mijini umefikia 90%
- Miradi mikubwa 1,633 ya usambazaji maji imekamilika
- Vituo vipya vya maji 107,819 vimejengwa
- Zaidi ya wananchi milioni 12 wamenufaika moja kwa moja
- Vijiji 196,160 vimefikiwa na huduma ya maji
Mageuzi haya yameiweka Tanzania kwenye ramani ya dunia kama mfano wa taifa linalowekeza kwa vitendo katika huduma za kijamii, hususan maji safi na salama.
Habari Zinazohusiana
UVCCM WILAYA YA KAKONKO WAFANYA MAADHIMISHO YA MIAKA 49 YA KUZALIWA KWA CCM
01 Feb, 2026
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Kakonko umefanya maadhimisho ya kipekee kuelekea miaka 49 ya kuzaliwa kwa CCM, yatakayofanyika rasmi tarehe 5 Februari 2026. Maadhimisho haya yamejumuisha shughuli mbalimbali za kijamii zenye lengo la kuunga mkono maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla.
ABUYA AWEKA MSISITIZO KWA VIJANA WA CCM KUKITETEA CHAMA NA VIONGOZI WAKE
31 Jan, 2026
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Kigoma, Ndugu Emanuel Abuya, amewataka vijana wa CCM kuendelea kuwa mstari wa mbele katika kutetea, kulinda na kudumisha misingi, sera na uongozi wa Chama Cha Mapinduzi, akisisitiza kuwa hilo ni jukumu la msingi na la kihistoria kwa jumuiya ya vijana.
UVCCM Mufindi yaadhimisha Miaka 49 ya CCM kwa Baraza maalum, yasifu Mchango wa Vijana katika kutafuta ushindi kwa CCM
31 Jan, 2026
Katika kuelekea maadhimisho ya miaka 49 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Wilaya ya Mufindi umeanza maadhimisho hayo kwa kufanya baraza maalum lenye lengo la kuwapongeza na kuwashukuru vijana wa chama kwa mchango wao mkubwa katika kazi ya kutafuta kura wakati wa Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba mwaka jana.