Chagueni Viongozi wanaojali amani na maendeleo endelevu ya taifa letu
18 Oct, 2025
10 Machapisho
Zanzibar, 17 Oktoba 2025
Uongozi wa Seneti wa Vyuo na Vyuo Vikuu Mkoa wa Magharibi, ukiongozwa na Mwenyekiti wake Ndg. Ikram Soraga, umeshiriki mafunzo ya elimu kwa mpiga kura katika Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Karume (KIST), yakilenga kuwaandaa wanavyuo kushiriki uchaguzi mkuu kwa amani ifikapo tarehe 29 Oktoba 2025.
Mafunzo hayo yametolewa na maafisa kutoka Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), ambapo Mgeni Rasmi, Ndg. Zeyana A. Hamid (Mbunge Mteule wa CCM Viti Maalum UWT – Kundi la Wasomi), amewasihi wanavyuo kudumisha amani, kuendelea kuchagua viongozi wanaohubiri maendeleo, na kuenzi mafanikio makubwa yaliyotekelezwa na Serikali ya CCM hususan katika sekta ya elimu, pamoja na mipango iliyoainishwa kwenye Ilani ya CCM 2025–2030.
Kwa upande wake, Ndg. Ikram Soraga aliwahimiza wanavyuo kuendelea kuwa na imani na Chama Cha Mapinduzi, kujitokeza kwa wingi kupiga kura, na kutokubali kushawishiwa na propaganda zinazolenga kuvuruga amani na umoja wa taifa.
#TokaNitokeTukatiki ✅
#KazinaUtuTunasongaMbele ✅
#ZanzibarMpya ✅
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.