SERIKALI KUKAMILISHA UJENZI WA CHUO CHA VETA KYAKA
15 Oct, 2025
8 Machapisho
🗓️ Tarehe 15 Oktoba,2025
📍Muleba-Kagera
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika Mkutano wa kampeni Uliofanyika Muleba, ameeleza dhamira ya Serikali kukamilisha ujenzi wa Chuo cha VETA Kyaka, hatua itakayowezesha vijana wa Kagera kupata mafunzo bora ya ufundi stadi na kujiajiri.
Amesisitiza kuwa chuo hicho kitakuwa sehemu ya mkakati wa serikali wa kuwawezesha vijana kupata ujuzi wa kisasa, kuongeza ajira na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika ukanda wa Ziwa, sambamba na kuijenga Tanzania yenye msingi wa ujuzi na ubunifu.
#OktobaTunatiki✅✅✅
#FyuchaBilaStresi
#TokaNitokeTukatiki✅
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.