SERIKALI YA CCM KUJENGA TAWI LA JKCI GEITA MJINI
🗓 13 Oktoba 2025
📠Geita Mjini
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea wa kiti cha Urais kupitia tiketi ya CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan akiinadi Ilani ya Chama cha Mapinduzi akiwa katika jimbo la Geita Mjini amewaeleza wananchi kuwa Serikali imejipanga kujenga tawi la JKCI ndani ya jimbo hilo ili kuwasogezea wananchi huduma ya matibabu ya moyo.
Hatua hii ni ushahidi tosha wa dira ya maendeleo ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya bila kikwazo cha umbali wala gharama kubwa, Ujenzi wa tawi la JKCI Geita Mjini utakuwa chachu ya mageuzi makubwa katika sekta ya afya ya mkoa huo, kwani utapunguza rufaa nyingi kwenda Dar es Salaam, kuongeza ajira kwa wataalamu wa afya na kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia huduma za kibingwa. Wananchi wa Geita sasa wanapaswa kuona hili kama ishara ya upendo wa kweli wa Serikali ya CCM kwao Serikali inayosikiliza, inayotekeleza, na inayoweka uhai wa wananchi wake mbele ya yote.
#OktobaTunatiki ✅✅✅
#FyuchaBilaStresi
#TokaNitokeTukatiki ✅
Habari Zinazohusiana
Mhe. Muhsin Ussi Ashiriki Ugawaji wa Vifaa vya Usafi Zahanati ya Kitunda Kuelekea Miaka 49 ya CCM
02 Feb, 2026
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Taifa (kundi la Vijana) na Mbunge wa Jimbo la Malindi, Mheshimiwa Muhsin Ussi, ameshiriki katika zoezi la kugawa vifaa vya usafi katika Zahanati ya Kitunda, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 49 ya kuzaliwa kwa Chama cha Mapinduzi (CCM).
UVCCM WILAYA YA KAKONKO WAFANYA MAADHIMISHO YA MIAKA 49 YA KUZALIWA KWA CCM
01 Feb, 2026
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Wilaya ya Kakonko umefanya maadhimisho ya kipekee kuelekea miaka 49 ya kuzaliwa kwa CCM, yatakayofanyika rasmi tarehe 5 Februari 2026. Maadhimisho haya yamejumuisha shughuli mbalimbali za kijamii zenye lengo la kuunga mkono maendeleo ya wananchi na taifa kwa ujumla.
UVCCM Ngome waadhimisha Kuzaliwa CCM kwa Vitendo, wasafisha Soko la Ngome Iringa
31 Jan, 2026
Vijana wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Tawi la Ngome, Kata ya Kihesa, Wilaya ya Iringa Mjini mkoani Iringa, wamefanya shughuli ya usafi wa mazingira katika Soko la Ngome kama sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya siku ya kuzaliwa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).