Dkt. Hussein Ali Mwinyi asema atayatekeleza Mambo Matatu Muhimu Kwa Vijana
10 Oct, 2025
15 Machapisho
Kusini Unguja, Zanzibar – Mgombea nafasi ya Urais wa Zanzibar kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameyataja mambo matatu ambayo atayatekeleza kwa vijana endapo atachaguliwa katika uongozi ujao.
Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza na vijana wa vyuo vikuu na makundi mbalimbali katika Chuo cha Mafunzo ya Vijana Tunguu, kilichopo Wilaya ya Kusini Unguja, mkoa wa Kusini Unguja.
Dk. Mwinyi amesema kuwa vijana wanahitaji fursa katika maeneo matatu muhimu: elimu, ajira na nafasi za uongozi.
"Tulipoingia tulikuta bajeti ya elimu ni shilingi bilioni 80 tu, sasa tumeongeza hadi shilingi bilioni 864, hivyo kipaumbele cha kwanza ni elimu ili vijana wetu waelimike. Kwa upande wa ajira, tumeahidi kutoa nafasi za ajira 350,000, na safari hii tutaongeza idadi hiyo zaidi kwa ajili ya vijana. Na fursa ya tatu ambayo vijana wanahitaji ni nafasi za uongozi, ambapo tutatoa nafasi za vijana katika uongozi wa serikali," alisema Dk. Hussein Ali Mwinyi.
Vijana waliohudhuria mkutano huo wameshuhudia kauli hizi kwa furaha kubwa, wakionyesha hamasa ya kushirikiana na Dk. Mwinyi kuhakikisha kwamba vijana wanapata fursa na ushiriki mkubwa katika maendeleo ya Zanzibar.
#KazinaUtuTunasongaMbele
#OktobaTunatiki
#TokaNitokeTukatiki
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.