🗓️BILA CCM MADHUBUTI NCHI YETU ITAYUMBA
10 Oct, 2025
22 Machapisho
📍 Tarehe 10/10/2025
⏰Butiama-Mara
Akiwa katika mkutano mkubwa wa kampeni uliofanyika leo Butiama Mkoani Mara, Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza kwa msisitizo mkubwa kuwa uimara wa Taifa letu unategemea Uimara wa CCM.
Amesema chama hiki kimekuwa nguzo kuu ya amani, umoja na maendeleo tangu kupatikana kwa uhuru, na bila misingi imara ya CCM, nchi inaweza kuyumba kisiasa na kiuchumi Dkt. Samia amewataka Watanzania wote kuendelea kukiamini na kukiunga Mkono CCM kwa vitendo, hasa kwa kujitokeza kwa wingi tarehe 29 Oktoba kumpigia kura ili kuendeleza safari ya maendeleo yenye Uthabiti, Utulivu na Matumaini Kwa Wote.
#OktobaTunatiki
#FyuchaBilaStresi
#TokaNitokeTukatiki
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.