Tafadhali subiri...
UMOJA WA VIJANA WA CCM (UVCCM)
UVCCM WILAYA YA CHAMWINO YAENDELEA NA ZIARA KATA YA CHILONWA | UVCCM
UVCCM WILAYA YA CHAMWINO YAENDELEA NA ZIARA KATA YA CHILONWA | UVCCM
Tafadhali subiri...
UMOJA WA VIJANA WA CCM (UVCCM)
Habari Nyingine

UVCCM WILAYA YA CHAMWINO YAENDELEA NA ZIARA KATA YA CHILONWA

25 Mar, 2026 00:00 Admin User 11 views 0 comments
Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Wilaya ya Chamwino umeendelea na ziara ya kiutendaji katika Kata ya Chilonwa leo tarehe 24/03/2026, ambapo Katibu wa Vijana amekutana na vijana wa eneo hilo kwa lengo la kusikiliza changamoto zao na kuimarisha shughuli za Jumuiya.
Katika ziara hiyo, Katibu alipata fursa ya kukusanya kero mbalimbali zinazowakabili vijana pamoja na kukagua maeneo yatakayotumika kwa ajili ya kutoa mafunzo mbalimbali (kambi) kwa vijana, hatua inayolenga kuwawezesha kiujuzi na kuongeza ushiriki wao katika shughuli za maendeleo.
Ziara hiyo inaendelea kuwa sehemu ya juhudi za kuimarisha uhai wa Jumuiya na kujenga msingi imara wa vijana wenye uwezo na ari ya kulijenga taifa.
Kazi na Utu Tunasonga Mbele
Taifa Letu, Amani Yetu
Admin User

Mwandishi wa UVCCM - Anatoa taarifa za kusisimua kuhusu shughuli za vijana na maendeleo ya taifa.