AHSANTE KAGERA KWA MAPOKEZI MAZURI YA ILANI YA CCM
17 Oct, 2025
10 Machapisho
📍Kagera - Tanzania
🗓️ Alhamisi16 Oktoba, 2025
Serikali ya Chama Cha Mapinduzi Chini ya Mwenyekiti wake Dkt Samia Suluhu Hassan ameendelea kuinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi ndani ya mkoa wa Kagera leo na kuahidi ahadi zifuatazo zilizopo kwenye ilani ya Chama Cha Mapinduzi ndani ya mkoa wa Kagera;
AFYA
Serikali ya Chama Cha Mapinduzi imejipanga kuboresha Huduma ya Afya kwa Nchi nzima kwa kutoa Bima ya Afya kwa watu wote ndani ya nchi itakayopelekea kupunguza vifo ndani ya Nchi.
Pia kwenye Sekta ya Afya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi imejipanga kwa siku 100 zijazo za kwanza baada ya Uchaguzi, kuwaajiri wataalam mbalimbali kwenye Sekta hii kwa lengo la kuboresha Sekta ya Afya.
ELIMU
Mgombea wa kiti Cha urais wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi yuko Dkt. Samia Suluhu Hassan ameahidi Uboreshaji wa Sekta Ya Elimu kwa kufanya ujenzi wa Mabweni kwa Shule za Sekondari, Na kutunisha mifuko Ya Elimu ya juu ili vijana wanaomaliza kidato cha Sita.
UMEME
Serikali ya CCM inaenda kumaliza Changamoto ya umeme kwa kujenga kituo cha kupokea na kupooza umeme ndani ya mkoa Wa Kagera ili kuwa na Umeme wa uhakika ndani ya masaa 24 kwa Mwaka.
#oktobatunatiki
#fyuchabilastresi
#tokanitoketukatiki
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.