SERIKALI KUKAMILISHA TAWI LA CHUO KIKUU CHA UDSM KAGERA
16 Oct, 2025
8 Machapisho
🗓️ Tarehe 16 Oktoba,2025
📍Bukoba Mjini-Kagera
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya CCM, Ndugu Samia Suluhu Hassan akiwa Bukoba Mjini, Mkoa wa Kagera, amesema kuwa Serikali itaendelea kuwekeza katika elimu ya juu kwa kukamilisha tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Kagera hatua itakayokuza fursa za elimu, kuongeza utafiti na kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Ukanda wa ziwa.
Amesema hatua hiyo ni sehemu ya dhamira ya Serikali kuhakikisha elimu bora inapatikana karibu na wananchi wote bila kujali umbali wala hali zao za kiuchumi, Aidha amesisitiza kuwa Uwepo wa chuo hicho Utachochea ajira, ubunifu na Maendeleo Endelevu katika Mkoa wa Kagera.
#oktobatunatiki✅✅✅
#fyuchabilastresi
#tokanitoketukatiki ✅
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.