SERIKALI CCM KULETA BOTI MBILI ZA KUSAFIRISHA WAGONJWA MULEBA
15 Oct, 2025
6 Machapisho
🗓️ Tarehe 15 Oktoba 2025
📍Muleba-Kagera
Katika kuimarisha huduma za afya kwa wananchi wanaoishi katika visiwa na Maeneo ya Mwambao wa Ziwa Victoria, Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza mpango wa serikali wa kuleta boti mbili mpya za kisasa kwa ajili ya kusafirisha wagonjwa katika Halmashauri ya Muleba, Mkoa wa Kagera.
Dkt. Samia amesema hatua hiyo Inalenga kupunguza Vifo vya mama Wajawazito na wagonjwa wanaoshindwa kufika Hospitalini kwa wakati, Sambamba na Kuendeleza jitihada za Awamu ya Sita za kuimarisha huduma za afya hadi katika maeneo ya mbali, Uamuzi huu unaonyesha dhamira ya kweli ya serikali ya CCM kuhakikisha hakuna Mtanzania anayepoteza maisha kwa sababu ya umbali au Ukosefu wa usafiri wa dharura hivyo kuendeleza falsafa ya maendeleo yenye kugusa maisha ya watu Moja kwa Moja.
#oktobatunatiki✅✅✅
#fyuchabilastresi
#tokanitoketukatiki ✅
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.