Tafadhali subiri ndugu...
UMOJA WA VIJANA WA CHAMA CHA MAPINDUZI

WAKIIONA HII CCM WANAPAGAWA..!!

kazi na utu tunasonga mbele,.

OKTOBA TUNATIKI

Uzalendo na Uongozi

Ziara ya Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Mkoani Geita .

KIJANI NA KIJANI

Uongozi na Uwajibikaji

Kazi na Utu, Tunasonga mbele.

KIJANI NA KIJANI

CCM hii tumeipenda wenyewe

Kazi na Utu, Tunasonga mbele.

KIJANI NA KIJANI

UONGOZI NA UZALENDO

Tnaandaa Viongozi wazalendo kwa maslai ya Taifa letu, leo na Kesho

Kazi na Utu, Tunasonga Mbele

KIJANA NA KIJANI

Tunazima zote, Tunawashakijana.

Tunasonga mbele pamoja
Kutana na Viongozi Wetu

Viongozi wetu wanaongoza kwa uadilifu na ujuzi kwa lengo la kuleta mabadiliko chanya kwa vijana wa Tanzania.

Mwakitinya

Mussa Mwakitinya(MNEC)

Naibu Katibu UVCCM bara

Rehema Sombi

Rehema Sombi

Makamu Mwenyekiti wa UVCCM

Kawaida

Ndugu.Mohammed Ali Kawaida (MCC)

Mwenyekiti UVCCM Taifa

Jokate

Jokate Mwegelo

Katibu Mkuu UVCCM

Abdi Mahmoud

Abdi Mahmoud

Naibu Katibu Mkuu UVCCM(Zanzibar)

Kuhusu Sisi

Jifunze kuhusu misingi mikuu inayoongoza Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi katika safari ya ujenzi wa taifa.

Historia Yetu

Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) ulianzishwa rasmi mwaka 1978, ukiwa ni muunganiko wa Afro-Shirazi Party Youth League (ASP-YL) ya Zanzibar na TANU Youth League (TYL) ya Tanganyika. Tangu kuanzishwa kwake, umekuwa chombo kikuu cha Chama katika kuandaa na kuwalea vijana kuwa viongozi na raia wema.

Kwa zaidi ya miaka 40 sasa, UVCCM imekuwa kiungo muhimu katika kuhakikisha kwamba sauti ya vijana inasikika katika mchakato wa kisiasa na maendeleo ya nchi. Umoja huu umejitolea kwa muda mrefu katika kukuza ujasiriamali wa vijana, uwezeshaji wa kiuchumi, na ustawi wa kijamii.

1978

Mwaka wa kuanzishwa kwa UVCCM baada ya muungano wa ASP-YL na TYL

5M+

Wanachama waliosajiliwa kwa sasa katika Umoja wa Vijana wa CCM

Imani ya UVCCM

Tunaamini kwamba binadamu wote ni sawa, na kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake. Imani yetu inajikita katika kuondoa aina zote za ubaguzi, unyonyaji, na rushwa, na kujenga jamii yenye usawa, haki, na amani.

UVCCM inaamini katika nguvu ya vijana kuleta mabadiliko chanya katika jamii. Tunasisitiza umuhimu wa:

  • Uzalendo na upendo kwa nchi na chama
  • Uwajibikaji na uadilifu katika utendaji kazi
  • Heshima kwa mwenendo wa kisasa wa kidemokrasia
  • Ushirikiano wa kitaifa na kimataifa
  • Maendeleo endelevu yanayolenga maslahi ya vizazi vya sasa na vijavyo

Itikadi Yetu

Itikadi ya UVCCM ni Ujamaa na Kujitegemea. Inasisitiza umuhimu wa kujenga uchumi imara unaomilikiwa na wananchi, huku serikali ikiweka mazingira wezeshi. Tunahimiza uzalishaji mali kwa pamoja na mgawanyo sawa wa matunda ya jasho la Watanzania.

Kwa mujibu wa itikadi hii, UVCCM inaongoza vijana katika:

Umoja na Ushirikiano

Kujenga mazingira ya ushirikiano na umoja kati ya vijana wa Tanzania bila kujali tofauti zao.

Ubunifu na Ujasiriamali

Kuhimiza ubunifu na ujasiriamali kati ya vijana kwa kuwapa fursa na mazingira wezeshi.

Elimu na Mafunzo

Kuhakikisha vijana wanapata elimu bora na mafunzo ya ujuzi wa kazi kwa soko la kazi.

Uhifadhi wa Mazingira

Kuhimiza utunzaji na uhifadhi wa mazingira kwa maendeleo endelevu ya nchi.

Malengo Makuu

UVCCM ina malengo makubwa ya kuhakikisha kwamba vijana wa Tanzania wanashiriki kikamilifu katika maendeleo ya nchi na kuwa viongozi wa kesho. Malengo yetu makuu ni:

  • Kuwaandaa vijana kuwa wanachama na viongozi waadilifu wa Chama Cha Mapinduzi.
  • Kuelimisha vijana juu ya Itikadi ya Chama na umuhimu wa uzalendo.
  • Kuwa chombo cha kuwaunganisha vijana wote nchini bila kujali tofauti zao.
  • Kuhamasisha na kushiriki katika shughuli za ujenzi wa taifa.
  • Kuhimiza na kukuza mipango ya uwezeshaji wa kiuchumi kwa vijana.
  • Kushirikiana na mashirika ya ndani na nje ya nchi kwa maslahi ya vijana.
  • Kuhakikisha vijana wanashiriki kikamilifu katika mchakato wa kisiasa na maamuzi ya kitaifa.
Ushiriki wa Vijana - 85%
Uwezeshaji wa Kiuchumi - 72%
Uelimishaji wa Itikadi - 90%
Ushirikiano wa Kimataifa - 68%

Muundo wa Uongozi

UVCCM ina muundo thabiti wa uongozi unaoanzia ngazi ya Taifa hadi ngazi ya mitaa. Muundo huu unahakikisha kwamba maamuzi yanafikiwa kwa ushirikiano na yanawaletea manufaa vijana wote.

  • Mwenyekiti wa Taifa

    Mohamed Ali Kawaida

    • Makamu Mwenyekiti

      Rehema Sombi

    • Katibu Mkuu

      Jokate Mwegelo

      • Naibu Katibu Mkuu (Bara)

        Mussa Mwakitinya

      • Naibu Katibu Mkuu (Zanzibar)

        abdi Mahamoud

Kamati ya Utekelezaji

Ni chombo cha juu cha kusimamia utekelezaji wa maamuzi ya Baraza Kuu na kuongoza shughuli za kila siku za Umoja huo kitaifa.

Baraza Kuu la UVCCM

Ni chombo cha juu cha maamuzi kinachojadili na kupitisha sera, mipango, na mwelekeo wa kisiasa wa UVCCM katika ngazi ya taifa.

Habari na Matukio
UVCCM Digital System

28 JULAI, 2025

CPA Makalla atangaza uteuzi wa awali wa wagombea ubunge CCM Majimbo 272

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetangaza rasmi uteuzi wa awali wa wagombea wa ubunge kwa majimbo yote 272 ya Tanzania Bara na Visiwani, huku jumla ya wagombea zaidi ya 5,000 wakijitokeza kuwania nafasi hizo, na zaidi ya 30,000 wakichukua fomu kuwania nafasi za udiwani.Kati ya wengi walioteuliwa ni Vijana, CCM imendelea kuwa na imani kubwa sana na Vijana . Zaidi, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo, CPA Amos Makalla, amesema uteuzi huo umefanywa na Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kwa kuzingatia sifa za wagombea, uwezo wa uongozi, kukubalika kwa wananchi na mahitaji ya kisiasa ya kila jimbo

Soma Zaidi
UVCCM Annual Meeting

27 JULAI, 2025

“Tutawateua Vijana” — Rais Samia Aonesha Imani, Mapenzi na Nguvu ya Vijana Ndani ya CCM

Mamia ya vijana kutoka mikoa yote wamehudhuria mkutano mkuu wa mwaka wa UVCCM uliofanyika Dodoma. Mkutano huo ulizungumzia mafanikio ya mwaka uliopita na kuweka mikakati ya mwaka ujao, ikiwa ni pamoja na mipango ya uwezeshaji wa kiuchumi na uongozi kwa vijana.Hatua hii ya Mwenyekiti wetu, Dkt. Samia, ni kwamba inatupa vijana nafasi,pia inatujengea uwezo na moyo wa kujiamini, kushiriki kikamilifu katika uongozi na maendeleo ya Taifa. Kwa kutupa nafasi za kugombea, CCM imeendelea kuonesha kuwa ni chama chenye mtazamo wa mbele, kinachotambua kuwa mustakabali wa Tanzania unategemea nguvu, ubunifu na ari ya vijana wake. Huu ni ujumbe thabiti kwamba chini ya uongozi wa Dkt. Samia, vijana ni sehemu ya maamuzi na mwelekeo wa Taifa letu.

Soma Zaidi
Tree Planting Campaign

05 JULAI, 2025

Kampeni ya Upandaji Miti Yavunja Rekodi

Zaidi ya miti milioni moja imepandwa nchi nzima katika kampeni ya UVCCM ya upandaji miti. Vijana wamejitolea kwa kiasi kikubwa katika shughuli hii ambayo inalenga kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kuhifadhi mazingira kwa vizazi vijavyo.

Soma Zaidi

Uko Tayari Kuleta Mabadiliko?

Jiunge na mamilioni ya vijana wazalendo katika safari ya ujenzi wa Tanzania imara na yenye maendeleo. Sauti yako ni muhimu, na UVCCM inaamini katika uwezo wako wa kuongoza na kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

Kuwa Mwanachama Sasa
Shuhuda za Vijana

Sikiliza kwa vijana wenzako waliofanikiwa kupitia mipango na mafunzo ya UVCCM

Mafunzo ya ujasiriamali niliyoyapata UVCCM yamenifungulia dunia na sasa naajiri vijana wenzangu 12 katika kampuni yangu ya utengenezaji wa viatu. Asanteni kwa msaada na mwelekeo mzuri.

Asha Mwinyi
Asha

Mjasiriamali, Zanzibar

Kupitia Darasa la Itikadi, nimejifunza maana halisi ya uzalendo na wajibu wangu kwa taifa. Sasa ninaweza kushiriki kwa ufahamu zaidi katika mjadala wa kisiasa na kuchangia maoni yangu kwa ujasiri.

David Molel
David James

Mwanafunzi, Arusha

Umoja huu unathamini mchango wa vijana kwenye kilimo. Tumepata fursa za kujifunza teknolojia mpya ya kilimo na sasa tunaweza kuzalisha zaidi kwa gharama ndogo na faida kubwa.

Jassica Mshama
Shafir Zubail

kutoka Dodoma

Sanaa ni ajira. UVCCM imetupa jukwaa la kuonyesha vipaji vyetu na kujipatia kipato. Sasa nina studio yangu na ninaweza kujikimu na familia yangu kupitia muziki.

Beka Beka
Beka Bakari

kutoka, Dar es Salaam

Mashindano ya UVCCM Cup yameniwezesha kufikia ndoto zangu za kucheza katika ngazi ya taifa. Sasa nimechaguliwa kuwa sehemu ya timu ya taifa ya mpira wa miguu ya wanawake.

Mwamba huyu hapa
stepehen James

Mwanamichezo, Mwanza

Ubunifu unapewa kipaumbele, na tunahimizwa kutatua changamoto za jamii yetu. Kupitia mradi wangu wa teknolojia, nimeweza kufanikiwa kutatua tatizo la usimamizi wa taka mjini.

Emanuel Ajaha
Emanuel ajaya

Mhandisi, Mbeya